Neema Ya Golgotha Lyrics By Papi Clever & Dorcas

Nilipofika Golgotha
Nikaiona huko
Neema kubwa kama mto, 
Neema ya ajabu. 

Neema ya Golgotha 
Ni kama bahari kubwa,
Neema tele na ya milele,
Neema ya kutosha! 

Nilipofika moyo wangu 
Ulilemewa sana, 
Sikufaamu bado vema 
Neema yake kubwa. 

Nilipoona kwamba Yesu 
Alichukua dhambi, 
Neema ikadhihirika, 
Na moyo ukapona. 

Mbinguni nitakapofika,
Furaha itakuwa
Kuimba juu ya neema
Milele na milele.